Thursday, May 30, 2013

MWILI WA MAREHEMU MANGWEA KUCHUNGUZWA NA JOPO LA MADAKTARI KABLA YA KUWASILI NCHINI


Marehemu Albert Mangwea (kulia)enzi za uhai wake, akiwa na M 2 The P ambaye yuko Hopitali bado, wasanii hao walikutwa wakiwa hoi katika chumba kimoja nchini Afrika Kusini.



PRETORIA, 
Afrika Kusini.

WAKATI utaratibu mzima wa mapokezi ya mwili wa marehemu Albert Mangwea, ukiendelea kufanyika huko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam nyumbani kwa Baba mdogo wa marehemu, taarifa kutoka Pretoria Afrika Kusini zinaeleza kuwa, mwili wa marehemu huyo utaanza kufanyiwa uchunguzi wa kina leo kabla ya kusafirishwa kuja nchini Tanzania.

Jamira Saidi anayeishi nchini Afrika Kusini alipozungumza kwa njia ya simu na Mwandishi wetu alisema kwamba, mwili wa marehemu leo utaanza kufanyiwa uchunguzi wa kina na jopo la Madaktari ili kujua sababu hasa ya kifo chake.


Jamira ambaye ni kati ya Watanzania waliojitolea kuhakikisha kwamba ukweli wa kifo cha msanii huyo unajulikana, tofauti na hivi sasa ambapo kila mtu anazungumza analo juwa.

Alisema wamekwisha fanya mawasiliano na serikali ya Afrika Kusini kuhusu uchunguzi huo.

"Mimi pamoja na baadhi ya Watanzania tunaoishi hapa Johanesburg na wengine waliopo Pretoria, tumeamua kufuatilia na kusimamia ukweli wa jambo hili, leo uchunguzi wa madaktari unaanza na tunatarajia kwamba utakamilika kesho na baada ya hapo tutaanza utaratibu wa kusafirisha mwili wa marehemu, kuja nyumbani Tanzania", alisema Jamira.

Akizungumzia hali ilivyo Afrika Kusini hivi sasa Jamira alisema kwamba hali imetulia ingawa watanzania wanaoishi katika maeneo mbalimbali nchini Afrika Kusini, wamepatwa na mshutuko kufutia kifo cha Mangwea.

Kila mtu aliyepata taarifa alijitahidi kuwasiliana na mwenzake na kupanga namna ya kukutana. Kuhusu hali ya msanii M 2 The P aliyekuwa amepoteza fahamu hadi jana jioni, Jamira alisema, hali yake kwa sasa ni nzuri madatkari wanaomtibu jana walitoa taarifa kwamba ameweza kufumbua macho na kuzungumza ingawa hawakusema alichokisema ila kwa ujumla hali yake imeanza kuwa nzuri.

























No comments: