Monday, May 27, 2013

RAIS BARACK OBAMA KUJA NA UJUMBE WA WATU 700 TANZANIA

Barack Obama.



Dar es Salaam, 
Tanzania.

RAIS wa Marekani, Barack Obama, atakuwa na ujumbe wa watu 700 katika ziara yake ya siku mbili nchini Tanzania kuanzia Julai Mosi mwaka huu.

Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema kutokana na ziara ya kiongozi huyo, alitoa wito kwa wafanyabiashara wenye hoteli, migahawa, magari ya kukodisha waziboreshe biashara zao ili Wizara hiyo iingie mkataba nao.

Aliongeza kuwa, akiwa nchini, Obama atafanya mkutano na viongozi wa nchi zinazoendelea kwa kuzungumzia umuhimu wa sayansi na teknolojia katika nchi zao.


“Ugeni huo ni mkubwa, ujio wa kiongozi huyu utaisaidia nchi kupata pesa za Miradi ya Changamoto za Milenia (MCC), ambazo zitatumika katika maji, elimu na barabara.

“Pia Rais Obama atazungumzia jinsi nchi za Afrika zitakavyopata umeme wa kutosha tofauti na sasa...kimsingi tumejiandaa katika mapokezi yake hata kwenye mavazi,” alisema Membe.

Hata hivyo Membe alisema tayari baadhi ya ujumbe ambao ataongozana nao umeanza kuwasili nchini kwa matayarisho.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Haule, alisema Umoja wa Nchi za Afrika (AU) sasa umefikisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake.

Alisema maadhimisho hayo yatafanyika Makao Makuu ya umoja huo Addis Ababa, nchini Ethiopia ambapo nchini Tanzania, yatafanyika viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam.

Aliongeza kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo nchini atakuwa Membe ambaye atakuwa na mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania.

Haule alisema umoja huo ulianza mwaka 1963 ambapo hadi sasa mafanikio waliyoyapata ni ongezeko la wanachama            kutoka 32 hadi 54, kupatikana kwa uhuru wa nchi ya Sudan    Kusini, viongozi wanawake barani Afrika na wananchi   kuwaheshimu viongozi wa nchi zao .

Alisema mbali ya mafanikio waliyopa ta pia kuna changamoto zilizopo katika nchi wanachama kama tishio la ugaidi, uharamia na halitete katika baadhiyanchi kama Somalia na Mali. (Source Majira News paper)

No comments: