Tuesday, May 7, 2013

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA ATEMBELEA LEO KANISA KATOLIKI LA OLASITI, LENGO KUZUNGUMZA NA WAUMINI NA VIONGOZI WA KANISA HILO, KUWAPA POLE

Waziri mkuu Mizengo Pinda akizungumza na Waumini wa kanisa katoliki la Olasiti Jijini Arusha leo, alikokwenda kutoa pole kufuatia mlipuko wa bomu la kutupwa kwa mkono, uliotokea kanisani hapo May 6 mwaka huu, na kusababisha vifo na majeruhi.(Picha na Mwandishi wetu).


Na Mwandishi wetu,
Arusha.

PAMOJA mambo mengine Waziri mkuu Pinda, aliwataka waumini wa kanisa hilo, katika kipindi hiki kigumu kuwa watulivu na kuendelea kumuomba Mungu, wakati serikali inaendelea na mchakato wa kulishughulikia tatizo hili.

Kadhalika Waziri huyo alilaani kitendo hicho cha kinyama kilichofanywa, na kuongeza kuwa serikali haitokubali kuendelea kuvumilia matukio kama haya kuendelea kutokea hapa nchini.

Mungu ibariki Tanzania, tuepushe na majanga kama haya wenye nia mbaya na nchi yetu, walaaniwe.

No comments: