Sunday, March 26, 2017

JESHI LA POLISI LATHIBITISHA KUKAMATWA KWA MSANII NAY WA MITEGO

Nay wa Mitego.
KAMISHNA msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro, Ulrich Matei ametoa sababu za kukamatwa kwa msanii Nay wa Mitego kwamba kunatokana na kutoa wimbo ambao amedai kuwa unaikashfu serikali ya awamu ya tano iliyopo madarakani.

Matei alifafanua kuwa wimbo huo ambao unaikashfu serikali hiyo unafahamika kwa jina la ‘Wapo’.

Alisema kuwa msanii huyo alikamatwa usiku wa kuamkia leo mkoani humo na kwamba shauri la Nay wa Mitego lipo Jijini Dar es Salaam, hivyo msanii huyo atasafirishwa na kupelekwa huko kwa ajili ya kuhojiwa kwa Mkuu wa Upelelezi wa mkoa huo.

Hata hivyo msanii huyo ambaye anafahamika kwa kutoa ngoma zenye ukakasi kwa baadhi ya watu amekamatwa leo akiwa mkoani humo, alipokuwa amekwenda kufanya show.



No comments: