Sunday, May 7, 2017

SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUTOKA KWA WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA KUFUATIA AJALI ILIYOPOTEZA MAISHA YA WANAFUNZI 32 HUKO KARATU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
WATANZANIA wenzangu, ninaungana na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, pamoja na Mheshimiwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kutoa pole nyingi sana kwa uongozi wa shule ya Lucky Vicent pamoja na wazazi wa watoto waliopoteza maisha kwenye ajali ya jana.

Mungu awape faraja katika kipindi hiki kigumu cha majonzi. Tuna muomba Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi.

Amina.
Mhe. Kassim Majaliwa (MB)
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


No comments: