Tuesday, September 1, 2015

MATUKIO MBALIMBALI YA ZIARA YA KAMPENI YA DOKTA MAGUFULI RUVUMA

Dokta John Magufuli akisalimiana na Dada ya wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi wilayani Nyasa, kupitia CCM na Mhamasishaji mkuu Marehemu Kapten John Komba alipokwenda kuweka shada la maua kwenye kaburi la Komba katika kijiji cha Lituhi wilayani humo wakati alipokuwa kwenye ziara yake ya kampeni.

Dokta John Magufuli akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Kapten John Komba.

Dokta John Magufuli akiomba dua na viongozi wenzake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mbele ya kaburi la marehemu, Kapteni John Komba kijijini Lituhi mkoani Ruvuma ambako alizikwa.

Dokta Magufuli akijinadi kwenye mkutano wa kampeni katika kijiji cha Lituhi wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma.

Dokta John Magufuli akimnadi mgombea ubunge CCM Jimbo la Nyasa, Stella Manyanya katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Lituhi wilayani Nyasa.

No comments: