Tuesday, September 1, 2015

DOKTA MAGUFULI AENDELEA KUPOKELEWA RUVUMA KWA KISHINDO

Mgombea Urais wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) John Magufuli, akiwapungia mikono wananchi waliowasili kwenye mkutano wa kampeni Mbinga mjini mkoani Ruvuma, ambapo aliahidi kuboresha kiwanda cha serikali cha kukoboa kahawa (MCCCO) na ujenzi wa barabara kiwango cha lami kutoka Mbinga mjini hadi Mbamba bay wilayani Nyasa.

Dokta John Magufuli akizungumza na wananchi wa Songea mjini mkoani Ruvuma, kwenye uwanja wa Majimaji ambapo aliwaeleza wananchi hao kuwa serikali yake itafanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.

Mgombea Urais kupitia tiketi ya CCM, Dokta John Magufuli akiwa na watoto ambao aliwapatia zawadi alipokuwa akiondoka baada ya kujinadi katika Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma.

No comments: