Monday, August 7, 2017

DOKTA MAGUFULI AREJEA JIJINI DAR ES SALAAM NA KUHUTUBIA UMATI WA WANANCHI ULIOMSIMAMISHA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE MKOANI TANGA

Baadhi ya wananchi wa eneo la Bunju wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli, wakati alipokuwa akizungumza aliposimama kwenye eneo hilo kuwasalimia wananchi hao wakati akirejea jioni ya leo Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoa wa Tanga.  
Watu wenye ujumbe wenye maneno ya aina mbalimbali nao hawakuwa mbali. 
Rais Dokta John Pombe Magufuli akimfariji mmoja wa wafanyabiashara wadogo waliopata changamoto eneo la Bunju A wilaya ya Kinondoni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Rais Dokta John Pombe Magufuli akishangiliwa na umati wa wananchi uliomsimamisha leo maeneo ya Bunju A wilaya ya Kinondoni nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.
Rais Dokta John Pombe Magufuli akiagana na umati wa wananchi uliomsimamisha leo maeneo ya Bunju A wilaya ya Kinondoni nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.
(Picha zote na Ikulu)

No comments: