Monday, June 29, 2015

NJOWOKA AENDELEA KUFUNIKA NYASA

Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma, Cassian Njowoka akipokelewa kwa shangwe na wanachama wa umoja huo kijiji cha Songambele kata ya Kihagara wilayani humo, wakati alipokuwa jana kwenye ziara yake ya kikazi kwa lengo la kuzungumza na wanachama hao.   

Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Cassian Njowoka akizungumza jana na wanaumoja huo katika viwanja vya kijiji cha Songambele kata ya Kihagara wilaya ya Nyasa mkoa wa Ruvuma, ambapo aliwataka wanachama wake kupenda kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo ili waweze kuondokana na umaskini.

No comments: