Saturday, January 28, 2017

RC RUVUMA AWATAKA NYASA KUJITUMA KATIKA KUFANYA KAZI ZA MAENDELEO

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt. Binilith Mahenge akizungumza na wananchi katika mikutano yake mbalimbali ya kuhamasisha maendeleo mkoani humo.
Na Kassian Nyandindi,   
Nyasa.

MKUU wa mkoa wa Ruvuma, Dkt. Binilith Mahenge amewataka wananchi waishio katika wilaya ya Nyasa mkoani humo kufanya kazi kwa bidii ili waweze kujiletea maendeleo yao, hatua ambayo itawasaidia kukuza uchumi katika familia zao na wilaya hiyo kwa ujumla.

Dkt. Mahenge alisema kuwa tabia ya uvivu na kutopenda kufanya kazi imepitwa na wakati na kwamba, ndiyo chanzo kikuu cha kuukaribisha umaskini kwa familia zao hivyo katika kukabiliana na hali hiyo hawana budi kila mmoja wao kutambua majukumu yao kwa kufanya kazi kwa malengo.


“Ni lazima tujenge tabia ya kujitegemea kufanya kazi kwa bidii, hatua ambayo itasaidia kuinua pato la mtu mmoja mmoja, wilaya, mkoa na taifa letu kwa ujumla hatutaki kuona vijana wetu wanatumia muda mwingi kucheza michezo ya Pool kwa serikali hii huu sio muda wake”, alisisitiza Dkt. Mahenge.


Hata hivyo alisema kuwa Tanzania ni nchi ambayo imekuwa ikisifika na mataifa mengine ya nje kutokana na kukua haraka uchumi wake na nguvu kubwa katika uzalishaji wa mazao mbalimbali ya chakula na biashara.

No comments: