Saturday, February 20, 2016

BENKI YA POSTA TANZANIA YAPONGEZWA KWA KUKARABATI VYOO VYA SHULE YA MSINGI MAKAMBI SONGEA


Ofisa uhusiano wa Benki ya Posta Tanzania, Noves Mosses   akifanya ufunguzi na makabidhiano ya vyoo vya shule ya msingi Makambi iliyopo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma. Ofisa huyo alisema kuwa  benki  hiyo imekuwa ikiunga mkono juhudi zinazofanywa na wananchi na serikali kwa ujumla katika kutatua changamoto mbalimbali kwenye sekta ya elimu, afya na ustawi wa jamii.
Na Kassian Nyandindi,

Songea.

BENKI ya Posta Tanzania (TPB), imepongezwa kwa hatua iliyochukua ya kufanya ukarabati wa vyoo vya wanafunzi wanaosoma shule ya msingi Makambi, iliyopo katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.
Wanafunzi shule ya msingi Makambi, wakifurahia.

Ukarabati huo uliofanywa, umeelezwa kuwa ni msaada mkubwa kwa watoto hao na kwamba itasaidia waweze kuwa na vyoo bora na kuepukana na magonjwa mbalimbali.
Shule ya msingi Makambi ina wanafunzi 850, ambapo imepata ufadhili wa kukarabatiwa vyoo hivyo, vyenye matundu 12 kwa thamani ya shilingi milioni 4.7. 

Ofisa uhusiano wa Benki ya Posta hapa nchini, Noves Mosses amekabidhi vyoo hivyo  kwa Mwalimu mkuu msaidizi  wa shule hiyo, Kanisius Ngongi baada ya kukamilika ukarabati wake.

Wanafunzi wa shule hiyo wamefurahia kukarabatiwa kwa vyoo hivyo, ambapo awali walisema kuwa walikuwa wakitumia choo kimoja wanafunzi wengi jambo ambalo lilikuwa ni hatari kwao kwa maambukizi ya magonjwa mbalimbali, hasa kwa watoto wa kike.

No comments: