Monday, February 15, 2016

MKURUGENZI WA KANDA MSD NA WENZAKE WASIMAMISHWA KAZI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.


Dar es Salaam,

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Kanda, huduma kwa wateja  Bohari kuu ya Dawa (MSD) hapa nchini, Cosmas Mwaifwani (pichani juu) na wenzake watatu kwa tuhuma za ubadhirifu wa shilingi bilioni 1.5.


Uamuzi huo wa Waziri ameutangaza leo Februari 15 mwaka huu, alipokuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, wakati akipokea shehena ya vitanda kutoka MSD ili kuweka kwenye jengo lililoelekezwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, libadilishwe matumizi yake kutoka kuhudumia maafisa wa Wizara ya Afya na kuwa wodi ya wazazi kwa lengo la kupunguza msongamano.

Wengine waliosimamishwa ni pamoja na Mkurugenzi wa fedha Joseph Tesha, Mkurugenzi wa ugavi, Misanga Muja na Mkurugenzi wa manunuzi, Henry Mchunga.

“Wote wanne wanasimaishwa kazi kuanzia leo hii, ili kupisha uchunguzi wa upotevu wa fedha hizi kiasi cha shilingi bilioni 1.5.”, alisema Waziri Ummy.

No comments: