Thursday, November 19, 2015

DOKTA TULIA NAIBU SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Dokta Tulia Mwansasu.


BUNGE la Jamhurio ya Muungano wa Tanzania, limepitisha jina la Dokta Tulia Mwansasu kuwa Naibu Spika wa Bunge, kwa kura 250 sawa na asilimia 71.2 dhidi ya mpinzani wake, Magdalena Sakaya aliyepata kura 101 sawa na asilimia 28.8.

Idadi ya Wabunge inayotakiwa ni 394, waliosajiliwa 369, akidi ni 184 na waliohudhuria ni 351 na hakukuwa na kura iliyoharibika.

No comments: