Friday, November 27, 2015

WAZIRI MKUU MAJALIWA AVAMIA BANDARINI AAMRISHA KUKAMATWA KWA MAOFISA TRA NA WENGINE KUFUKUZWA KAZI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akikabidhi leo orodha ya makontena yaliyopotea bandarini na ambayo TRA haina taarifa zake.


Na Mwandishi wetu,
Dar es Salaam.

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa Maofisa kadhaa wa Mamlaka ya Mapato hapa nchini (TRA) na wengine kufukuzwa kazi, baada ya kufanya ziara ya kushitukiza bandarini Jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo iliyochukuliwa na Waziri Mkuu, imefuatia baada ya kukuta madudu ambayo hakuyafurahia na yanadaiwa kufanywa na baadhi ya watendaji wa TRA.

Maofisa hao ambao majina yao yamehifadhiwa, ili Jeshi la Polisi lianze kazi ya kuwashughulikia wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.

Utekelezaji huo umekuja baada ya kubainika kwamba, kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya bandari (TPA) inazo, lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.

No comments: