Wednesday, March 16, 2016

WAKUU WA MIKOA WAAGIZWA KUKUSANYA MAPATO KIKAMILIFU

Suleiman Jaffo.


Dar es Salaam.

NAIBU waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Suleiman Jaffo amewataka Wakuu wa mikoa hapa nchini, kuhakikisha kwamba wanasimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato ndani ya mikoa yao, ili fedha hizo ziweze kutatua matatizo ya wananchi yaliyopo katika mikoa yao.

Waziri huyo alisema hayo leo alipokutana na wakuu wapya wa mikoa, kabla ya kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi huku akiongeza kuwa kwa muda mrefu kumekuwa na uzembe katika ukusanyaji mapato, hali ambayo inachangia mikoa mingi kushindwa kutatua matatizo yao binafsi na kutegemea msaada toka serikali kuu.

Pamoja na mambo mengine, amewataka wakuu hao wa mikoa, kushirikiana kikamilifu na watendaji wa mikoa yao, ili waweze kufanya kazi pamoja na endapo kutakuwa na ubadhirifu wowote wakuu hao wa mikoa wasifumbie macho, vitendo hivyo.

No comments: