Monday, September 18, 2017

BALOZI WA FINLAND ASHANGAZWA NA VIVUTIO VYA UTALII ZIWA NYASA

Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

MSHAURI na Mwakilishi wa Balozi wa Finland nchini Tanzania, Kari Leppanen amefanya ziara ya siku mbili Mwambao mwa ziwa Nyasa mkoani Ruvuma.
Mwakilishi wa Balozi wa Finland Tanzania, Kari Leppanen.

Akihojiwa juzi kwenye Hoteli ya kitalii ya Watawa wa Mtakatifu Vincent iliyopo katika fukwe za Kilosa mjini Mbambabay wilayani humo, alisema kuwa ameshangazwa na vivutio vya utalii ambavyo ni vya kipekee na adimu havipatikani sehemu nyingine yoyote Duniani vilivyopo katika ziwa hilo.

Balozi huyo alisisitiza kuwa iwapo vivutio hivyo vikiendelezwa vitafungua fursa kubwa ya uwekezaji na utalii kwa wananchi wa eneo hilo na mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.


Miongoni mwa vivutio vilivyopo katika ziwa Nyasa ni fukwe za asili, visiwa ambazo samaki wa mapambo aina zaidi ya 400 huzaliana kwa wingi, milima ya Livingstone, mawe ya ajabu kama vile jiwe la Pomonda na vivutio vingine vya Ikolojia na Utamaduni.

No comments: