Friday, September 29, 2017

MATUKIO KATIKA PICHA USALAMA BARABARANI SONGEA

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani (RTO) mkoa wa Ruvuma, Abel Swai akikagua daladala yenye namba T 657 BEZ linalofanya safari zake kati ya Songea mjini hadi kijiji cha Mtakanini wilayani Namtumbo mkoani humo, ambapo magari hayo hubainikia kuwa na matatizo mbalimbali ikiwemo ubovu na wafanyakazi wake kutokuwa na sare wanapofanya kazi hiyo ya kusafirisha abiria.
Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Ruvuma, Abel Swai akitoa elimu ya usalama barabarani kwa mwendesha baiskeli ambaye alikutwa akitembeza mkaa barabarani bila kufuata taratibu na sheria za usalama barabarani, jambo ambalo limekuwa ni chanzo cha kuongezeka kwa matukio mengi ya ajali zinazotokea mkoani humo. sha abiria. (Picha zote na Muhidin Amri)

No comments: