Sunday, March 25, 2018

MNADA WAINGIZA MAMILIONI YA FEDHA MANISPAA SONGEA

Baadhi ya mitambo mbalimbali na  magari yaliyopigwa mnada na Manispaa Songea Mkoani Ruvuma.

Na Kassian Nyandindi, 
Songea.

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, Machi 24 mwaka huu imeuza kwa njia ya mnada wa hadhara mitambo yake 16 ikiwemo magari, pikipiki na mitambo mingine chakavu na kufanikiwa kukusanya zaidi ya Shilingi Milioni 87.75.

Mitambo hiyo ambayo imeuzwa katika mnada huo ni Mitsubishi Bozer, Toyota land Cruiser station wagon mbili, Nissan station wagon, Nissan station wagon tipper, Isuzu tipper mbili, Hyster Roller, pikipiki sita aina ya Suzuki 125, pikipiki aina ya Honda 110 na Hysosung.

Fedha hizo taslimu ambazo zimekusanywa katika mnada huo uliofanyika kwenye Karakana ya Manispaa ya Songea na kusimamiwa na Kampuni ya YONO Auction Mart chini ya dalali mahiri, Zuberi Lumbizi ni shilingi zaidi ya milioni 26.


Kiasi hicho cha fedha taslimu kilichopatikana ni moja ya masharti ya mnada ambapo Mnunuzi alitakiwa kulipa amana ya fedha taslimu sio chini ya asilimia 25 ya thamani ya gari, pikipiki au mtambo atakaoununua na kukamilisha malipo yote katika muda wa siku 28 kuanzia tarehe ya mnada.

No comments: