Friday, October 16, 2015

BREAKING NEWS: MGOMBEA UBUNGE DEO FILIKUNJOMBE AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA CHOPA

Mbunge wa Ludewa mkoani Njombe, Deo Filikunjombe aliyevaa shati la kijani enzi ya uhai wake akishiriki na wananchi wake katika shughuli mbalimbali za maendeleo Jimbo la Ludewa.
HABARI ZILIZOTUFIKIA HIVI PUNDE:

ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Ludewa mkoani Njombe na mgombea wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Deo Filikunjombe (Pichani) amefariki dunia wakati akielekea kwenye jimbo lake akitokea jijini Dar es Salaam, akiwa kwenye Chopa iliyoanguka jana katika hifadhi ya wanyama ya Selous iliyopo mkoani Morogoro. 

Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, na kwamba hakuna mtu aliyepona katika ajali hiyo.

No comments: