Friday, October 2, 2015

MWANAFUNZI SHULE YA MSINGI MAHELA MBINGA AOMBA MSAADA AKATIBIWE INDIA

MAELEZO YA PICHA HII:

Huyu ni mtoto Yasin Ngonyani mwenye umri wa miaka 13, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita shule ya msingi Mahela wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, anaomba msaada wa kuweza kufanikiwa kwenda nchini India kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya oparesheni ya mguu wake ambao unamsumbua kwa muda mrefu sasa.

Kwa mujibu wa Madaktari ambao wamemfanyia uchunguzi wa awali, gharama za matibabu yake ni shilingi milioni 17, hivyo yeyote atakayeguswa na tatizo hilo ambaye yupo tayari kumsaidia kuweza kufanikisha matibabu ya mguu huo, anaweza kuwasiliana na mzazi wake kwa simu namba; 0763 - 770387 au 07 - 12345831.

Hata hivyo kwa mawasiliano zaidi unaweza kupiga simu namba; 0754 - 236443 kwa Ofisa ustawi jamii, Davina Maketa hapa wilayani Mbinga ambaye ndiye anafuatilia kwa karibu na kushughulikia matibabu ya mtoto huyo.

KUTOA NI MOYO SIO UTAJIRI !!


No comments: