 |
IGP Said Mwema |
Na
Mwandishi wetu,
Tanga.
AJALI
mbaya iliyotokea jana wilaya ya Handeni mkoani Tanga na kusababisha vifo vya
watu watatu, ambao ni waandishi wa habari wawili kutoka kampuni ya Mwananchi
Communication na gazeti la Uhuru na Mzalendo, Radio Aboud na Ofisa Uhamiaji wa
wilaya hiyo.
Ajali
hiyo iliyotokea Aprili 11 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi iliuhusisha
msafara wa Mkuu wa wilaya hiyo Muhingo Rweyemamu, ni msafara unaodaiwa kuwa
ulikuwa na magari matatu tu lakini gari moja liliacha njia na kupinduka.
Waliofariki
ni pamoja na Hussein Semdoe mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Hamis Bwanga wa
Radio Uhuru na Abood pamoja na Mariam Hassan ambaye ni Ofisa Uhamiaji wilaya ya
Handeni.
Mkuu
wa wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo
pamoja na vifo vya marehemu hao.
Akizungumza
na Mwandishi wetu, Mkuu wa wilaya hiyo alisema ajali hiyo ilitokea wakiwa
kwenye msafara, kuelekea Ndolwa kupanda miti.
Muhingo
alieleza kwamba gari lililopata ajali ni la Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Handeni, lenye namba za usajili STJ 4673 ambalo ndilo lililokuwa likitumiwa na
Ofisa Uhamiaji, Hassan pamoja na wanahabari hao.
Alisema
huu ni msiba mkubwa kwa wilaya ya Handeni kwani wamepoteza wachapakazi na
watu muhimu katika mchakato wa maendeleo ya wilaya hiyo.
"Wilaya
ya Handeni imepoteza wanahabari kwa asilimia 100, kwani waandishi hawa ndiyo
walikuwa wanahabari pekee wilayani hapa,
"Msiba huu ni mkubwa si kwa tasnia ya
wanahabari pekee bali hata kwa juhudi za maendeleo ya wilaya ya Handeni,
tulikuwa tukizunguka nao katika shughuli mbalimbali hapa wilayani hivyo ni pigo
kubwa," alisema Muhingo.
Aidha
Mkuu wa wilaya hiyo alisema marehemu Hassan ambaye alikuwa afisa uhamiaji kabla
ya umauti alikuwa mpambanaji mkubwa wa wahamiaji haramu katika wilaya hiyo.
Aliongeza
kuwa hivi karibuni alifanikiwa kuwakamata takribani wahamiaji 70 eneo hilo, hivyo kifo chake ni
pigo kubwa kwa nguvu kazi ya wilaya ya Handeni.
Miili
ya waandishi imechukuliwa na ndugu na kwamba serikali inatoa pole kwa ndugu na
jamaa waliopatwa na matatizo hayo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa
Tanga Costantine Massawe amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo.