Friday, January 19, 2018

SERIKALI YATOA TAHADHARI KUHUSU UGONJWA HATARI WA CHIKUNGUNYA

Ummy Mwalimu.


SERIKALI hapa nchini kupitia Wizara yake ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa tahadhari kuhusu ugonjwa wa Chikungunya ambao umeripotiwa na vyombo vya habari kutokea Mombasa nchini Kenya.

Waziri wa Wizara hiyo, Ummy Mwalimu ametoa taarifa yake leo Januari 19 mwaka huu akisema kuwa mpaka sasa Shirika la Afya Duniani (WHO) bado halijatoa taarifa rasmi lakini Serikali hapa nchini inatoa tahadhari kuzingatia muingiliano mkubwa wa watu baina ya nchi hizi mbili Kenya na Tanzania.

Kwa ujumla Wizara ya afya imefafanua kuwa ugonjwa wa Chikungunya unasababishwa na kirusi ambacho kinaenezwa na mbu aina ya Aedes na kusema ugonjwa huo si mgeni nchini Tanzania kwani ulishawahi kutokea.

Taarifa zaidi hii hapa;







No comments: