Thursday, January 18, 2018

SIMBA YAMTANGAZA RASMI KOCHA MPYA

Pierre Lechantre.


KLABU ya Simba leo imemtangaza rasmi Mfaransa Pierre Lechantre, kuwa Kocha mpya atakayekinoa kikosi hicho, ambacho kilikuwa hakina mwalimu baada ya kumfukuza aliyekuwa kocha wake, Joseph Omog mwishoni mwa mwaka jana.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Klabu hiyo, Haji Manara imeeleza kuwa kocha huyo ataanza kazi mara moja na atasaidiwa na kocha msaidizi wa sasa Masoud Djuma.

Masoud ambaye alikuwa akikaimu nafasi hiyo, na kwamba Mfaransa huyo atashuhudia mchezo wa Simba SC dhidi ya Singida United leo Januari 18 mwaka huu katika uwanja wa Taifa.


Mfaransa huyo alishawahi kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Cameroun kilichoshinda ubingwa wa Afrika mwaka 2000 na ameshawahi kushinda tuzo ya kocha bora wa bara la Afrika 2001.

Soma zaidi taarifa hiyo kutoka Simba SC;

TAARIFA KWA UMMA

Klabu ya Simba inayofuraha kubwa kuwajulisha Wanachama na washabiki wake kwamba imempata kocha wake mkuu mpya, Mfaransa Pierre Lechantre.

Kocha huyo mzoefu ataanza kazi mara moja na atasaidiwa na kocha msaidizi wa sasa Masoud Djuma ambaye alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Kocha Lichantre keshawahi kufundisha vilabu kadhaa duniani kikiwemo kikosi cha timu ya Taifa ya Cameroun kilichotwaa ubingwa wa Africa 2000.

Kocha huyo pia alipata kuwa kocha bora wa Afrika mwaka 2001 na pia barani Asia mwaka 2012.

Lechantre amekuja pia na kocha wa viungo Mmorocco Mohammed Aymen Hbibi, na leo jioni kocha Lechantre ataishuhudia Simba ikicheza na Singida United kwenye Uwanja wa Taifa.

No comments: